China Yasitisha Kwa Muda Wageni Kuingia Nchini Huko ili kukabiliana na Corona

China imetangaza kuzuia wageni wote kuingia nchini humo hata kama wana viza au vibali, lengo likiwa kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona.

China pia imeagiza ndege za nchi hiyo na zile za kigeni kufanya safari moja tu kwa wiki na hazitakiwi kujaza watu kwa zaidi ya asilimia 75.

Taarifa kutoka China zimeeleza kuwa kulikuwa na wagonjwa 55 nchini humo siku ya Alhamisi, kati yao 54 walikuwa ni wa kutoka nje ya nchi hiyo.




from MPEKUZI

Comments