Tafsiri 17 Kuhusu Kuota Ndoto Upo Shuleni Unasoma Au Upo Shuleni Unafanya Mtihani Wakati Ulishamaliza Shule Miaka Mingi Iliyopita

IMESIMULIWA  NA   Dokta  Mungwa  Kabili…………………………………0744 -  000  473.


Awali  ya  yote  ujumbe  katika  ndoto  yoyote  ile  huwa  unapatikana MWISHONI  mwa  ndoto  wakati  ndoto  inaisha  na  sio  MWANZONI  mwa  ndoto,

KUHUSU  KUOTA  UMERUDI UTOTONI AU  SHULENI  UNASOMA  WAKATI  SHULE  ULISHA  MALIZA  ZAMANI.

Hii  ni ndoto  ambayo  imekuwa  maarufu  sana  katika  siku  za  hivi  karibuni.  Siku  hizi  karibu  kila  mtu mzima   anaota  ndoto  hii.  Sio  mara  moja  wala  sio  mara  mbili  ni  mara  nyingi  nyingi.

Wapo  wanao  ota  ndoto  hii  walau  mara moja au mbili  kila mwezi, wengine  huota  mara  moja  kila  wiki  na  wengine  huota  karibu  kila  siku.   Wakati mwingine  mtu  anaweza  kuota  ndoto  hii Zaidi  ya mara  moja  ndani  ya  usiku  mmoja  na  hali  hiyo  inaweza  kujirudia   mfululizo, yani  mtu  amelala  tuseme  saa  nne  usiku , saa  sita  usiku  anaota  ndoto  hiyo, anastuka. Akilala  tena  anaiota  ndoto  hiyo hiyo.


NINI  MAANA  YA  NDOTO  HIZI  MBILI ; KUOTA  UPO  SHULENI  UNASOMA  AU  UPO  UTOTONI  NA  KUOTA  UPO  SHULE  UNAFANYA  MTIHANI  AMBAO  ULISHA  UFANYAGA  MIONGO  KADHAA  ILIYOPITA  AU  MIAKA  MINGI  ILIYOPITA  ?

Tuanze  na  ndoto  ya  kuota   UPO  SHULENI  UNASOMA  WAKATI  WEWE  ULISHAMALIZAGA  SHULE  MIAKA  MINGI  SANA  IMEPITA.

Ulimaliza  darasa  la  saba  mwaka  1994  na  kuendelea  na  masomo  ya  juu. Sasa  hivi  umeshakuwa  mtu  mzima mwenye  watoto  na  pengine  wajukuu  kabisa.   Lakini  unalala  usiku  unaota  ndoto  umerudi  shuleni  katika  darasa  hilo  hilo  la  saba  au  hata  chini  ya  hapo. Upo   katika  mazingira ya  shule  ulio  kuwa  unaisoma.  Katika  ndoto yako  hiyo  mazingira  ya  shule  yako  huwa  ni  yale  yale  yaliyo  kuwepo  kipindi  unasoma hata  kama  katika  ulimwengu  wa  nyama  yameshabadilishwa. Mfano  kulikuwaga  na  miti  mikubwa  labda  sasa  hivi  imeshakatwa.  Kulikuwa  na  sehemu  ya  wazi  na sasa  hivi  imejengwa  madarasa  mengine.  Wewe  katika  ndoto  yako  utakuwa  katika  mazingira  yale  yale  yaliyo  kuwepo  mwaka  huo  wa  94  wakati  bado  unasoma  katika  shule  hiyo.

JE   NDOTO  HII INA  MAANA  GANI  ?
Dhana  iliyo  jengeka  miongoni  mwa  watu wengi katika  jamii  ni  kwamba  ukiota  ndoto  hii  basi  maana  yake  ni  kwamba  kuna  watu  wanakurudisha  nyuma  kwa  kutumia  uchawi.  Yani  kwa  lugha  nyepesi  kuna  watu  wanakufunga  kichawi  ili  usipate  maendeleo. Uendelee  kubakia  hapo  hapo  ulipo  na  uzidi  kurudi  nyuma  kimaisha.

JE  TAFSIRI  HII  NI  SAHIHI  ?
Jibu  langu  ni  NDIO  na  HAPANA.  Ndio  kwa maana   ya  kwamba  ukiota  ndoto  umerudi  shuleni  inaweza  kuwa  ina  maanisha  kwamba  kuna  watu  wanakufunga kwa  lengo  la  kukurudisha  nyuma  kimaendeleo  lakini  HAPANA  kwa  maana  ya  kwamba  si  kila  unapo  ota  ndoto  umerudi  shuleni  basi  tafsiri  yake  ni  kwamba  kuna  watu  wanakuroga  kwa  lengo  la  kukufunga  ubaki  hapo  hapo  ulipo  na  kukurudisha   nyuma.

Ndoto  hii  ina  tafsiri  nyingi  sana. Kuipa  tafsiri  moja  tu  kama  watu  wengi  wanavyo  amini  ni  kuto  kuitendea  haki  ndoto  hii  na  ulimwengu  wa  ndoto  kwa   ujumla  wake.

Kama  nilivyo  dokeza  hapo  juu, ndoto  hii  ina  tafsiri  nyingi  sana.  Baadhi  ya  tafsiri  muhimu  kuhusu ndoto  hii  ni  kama  ifuatavyo ;

TAFSIRI NAMBA MOJA :       UNAPEWA  ONYO  KUHUSU  MWENENDO  NA TABIA  ZAKO  AMBAZO  ZINAKURUDISHA  NYUMA  KIMAENDELEO.

Ulevi, uzinzi  na  uasherati  pamoja  na  anasa  za  dunia  ni  miongoni  mwa  tabia  na  mienendo  ambayo  inarudisha  nyuma  maendeleo  ya  watu  wengi  sana . kama  wewe  unajihusisha  na  tabia  hizo  hapo  juu  halafu  ukawa  unaota  ndoto umerudi  utotoni basi ni ishara  kwamba  tabia  na  mwenendo  wako  vinakurudisha  nyuma  kimaendeleo.  Tabia  na  mwenendo  wako  ndio  mchawi  wako  namba  moja.

 2.TAFSIRI   NAMBA  MBILI :   NI  ISHARA  YA KUKUONDOA  HOFU  JUU  YA  JAMBO  ULILO  LIFANYA  AU  LILILO  KUTOKEA  AMBALO  LIMEKUFANYA  UWE  NA  HOFU  KUBWA  SANA  KATIKA  MAISHA  YAKO.

Mfano   umekutana  kimwili  na  mtu  bila  kutumia  kinga  halafu  baadae  ukasikia  mtu  huyo aliwahi  kuwa  na  mahusiano  ya  kimapenzi  na muathirika, jambo  hili  linaweza  kukupa  hofu  kubwa  sana  kwenye  nafsi  kiasi  cha  kukata  tamaa  ya  kuishi  duniani  kwa  kuamini  na  wewe  umeathirika  na  mwisho  wa siku  unaweza  kujiingiza  katika  tabia  za  hatari zaidi  kama  kuendelea  kufanya  ngono  nzembe  na watu  mbalimbali  huku  ukiamini  kwamba  wewe  ndio  unawasambazia . Matokeo  yake  basi  katika  mchakato  huo  wa  kuwaambukiza  na  kuwasambazia  watu  virusi, wewe  ndio  unaweza  ukajikuta  unaambukizwa.  Malaika  walinzi wako  kwa  sababu  wana  uwezo  wa  kusoma  nyota  yako  na  kujua  mambo  yatakayo  kutokea  mbeleni, wataanza  kukupa  ujumbe  wa  kukutoa  hofu  kwa  njia  ya  ndoto. Ukiwa  katika  hali  kama  hii  halafu  ukaanza  kuota  ndoto  umerudi  utotoni  basi  maana  yake  ni  kwamba  jambo  unalo  lihofia  halipo.  Yani  kwa  suala  la usalama  wa  damu  yako, damu  yako  ni  salama  kama ilivyo  kuwa  miaka  mingi  iliyo  pita  wakati  upo  utotoni.   Hapa  malaika  walinzi  wako wanakuwa  wameisoma  nafsi  yako  ambayo  inatamani  siku  zirudi  nyuma.  Hivyo wanakujibu  kwa  njia  ya  ndoto  kwa  kukurudisha  nyuma  kwa  njia  ya  ndoto.

Hapa  malaika  walinzi  wako  wakiona  huelewi  kwa  njia  ya  ndoto, wataanza  kukupa  ishara  nyingine  za  kawaida. Kwa  mfano  uta kuwa  unatembea  mjini  mara  unakutana  na  rafiki  yako  ambae  mlisoma  wote  shule  ya  msingi  na  kwa  mara  ya  mwisho  mlionana  miaka  kumi  iliyopita  ( kipindi  ambacho  hukuwa  na  hofu  kama  uliyo  nayo  leo hii ). Unatoka  hapo  unaenda  kupanda  kwenye  gari  unasikia  zinapigwa  nyimbo  za  miaka  25  iliyo  pita  wakati  upo  darasa  la  tatu  nakadhalila . ( Ukiona  hivyo  basi jua  unapewa  taarifa  kwamba  jambo  unalo  lihofia  halipo  wala  halijakutokea  kwa  hiyo usiwe  na  hofu  yoyote  kuhusu  jambo  hilo )

4.TAFSIRI  NAMBA  NNE :  UNAPEWA  ONYO  USIRUDIANE  NA  MTU  ULIE  KUWA  UMEACHANA  NAE.

Ulikuwa  na  mke, mume , mchumba  au  mpenzi  halafu mkatengana.  Baada  ya  muda  Fulani, mke, mume, mchumba  au  mpenzi  huyo  akakuomba  mrudiane.  Ukiwa  katika  mchakato  wa  kutaka  kurudiana  nae  unaanza  kuota  ndoto umerudi  shuleni  au  utotoni.  Tafsiri  ya  ndoto  hiyo  ni  kwamba  endapo  utarudiana  na  mke, mume, mchumba  au  mpenzi  huyo  basi  jambo  hilo  litakurudisha  nyuma  sana  kimaisha.  Malaika walinzi  wako  kwa  sababu  wana  uwezo  wa  kuona  mambo  yatakayo  kutokea  mbeleni  wanakupa  tahadhari  hiyo  kwa  njia ya  ndoto.

Sababu  zinaweza  kuwa  mke, mume, mpenzi, au  mchumba  huyo  ana  laana  na  vifungo  vya  kimasikini  vya  ukoo, familia  au  kijiji.  Ukifunga  nae  ndoa  au  ukiwa  nae  katika  mahusiano  ya  kimapenzi  maana  yake  na  wewe  unakuwa  umeunganishwa  kwenye  laana  na  vifungo  vyake.

Vile  vile  sababu  zinaweza  kuwa  tabia  za  mwanaume  huyo zitakurudisha  nyuma  kimaendeleo.  Kwa  mfano  inawezekana  wewe  unafanya kazi  au  shughuli  inayo  kuingizia  kipato  ambacho  unakitumia  kukidhi  haja  zako  na  kuwasaidia  familia  yako halafu  huyo  mwanaume  yeye  hataki  kuoa  mwanamke   ambae  anafanya  kazi.  Yeye  akikuoa  atataka  uwe  mama  wa  nyumbani. Atakuachisha  kazi  na  hatotaka  ufanye  biashara  yoyote  na  anaweza  kutumia  fursa  hiyo  kukunyanyasa  pia  na  mwisho  wa  siku  utaishia  kuachana  nae  huku  ukiwa  umepoteza  muda  wako  mwingi  sana ukiwa  nae. NDIO  MAANA  UNAPEWA  ONYO  USIRUDIANE  NAE.


5. TAFSIRI NAMBA  TANO : NI  ISHARA  KWAMBA  MARADHI  YA  KICHAWI  YALIYO KUWA  YANAKUSUMBUA  YAMEPONA.

Kama  ulikuwa  umetupiwa  maradhi  ya  kichawi  na  yakakutesa  kwa  muda  mrefu  halafu  baadae  ukapata  tiba  ya  kuondosha  maradhi  hayo basi  kuna  uwezekano  mkubwa  sana  kuota  ndoto  umerudi  utotoni.

Hii  maana  yake  ni  kwamba, maradhi  yako  yote  yameondoshwa  na  sasa  umekuwa  mpya.  Umerudi  kwenye  upya.,  Kwa  hiyo  kama  upo  kwenye  kundi  hili  halafu  ukaota  ndoto  umerudi  utotoni  basi  maana  yake  ni  kwamba  wewe  umekuwa  mpya.

6.TAFSIRI NAMBA  SITA : NI ISHARA  KUWA  NYOTA  YAKO  ILIYO  KUWA  IMEIBIWA AU  KUCHAFULIWA SASA   IMERUDISHWA.

Kama  nyota  yako  ilikuwa  imechukuliwa  halafu  ikarudishwa  basi  kuna  uwezekano  mkubwa wa  wewe  kuota  ndoto  umerudi  utotoni.

 Hii  maana  yake  umekuwa  mpya. Nyota  yako  imekuwa  swafi  kama  ulivyo  kuwa  mtoto  mdogo.   Ukiachilia  mbali  kurogwa, nyota ya  mtu  huwa  ina  haribiwa  na  zinaa.  Unapo fanya  zinaa  una  haribu  nyota  yako  kwa  sababu  una unganisha  nafsi( nyota )  yako  na  nafsi ( nyota ) ya  mtu  unae  fanya  nae  zinaa.  Katika  ulimwengu wa  kiroho, watoto wadogo ni  alama  ya  nyota  inayo  ng’aa  ama  nyota  iliyo  kamilika, nyota  safi.

Sasa  kama  nyota  yako  ilikuwa  imechafuliwa, imekufa, imeshushwa, imefungwa  au  ime imechukuliwa ( imeibwa )  halafu ukarejesha  nyota  yako. Ukiota  ndoto  umerudi  utotoni  maana  yake  ni  kwamba  nyota  yako  iliyo  kuwa  imeibwa  sasa  imerudi.  Na  kama  wewe  ni  mwanamke  basi  tunasema  umerudi  kwenye  ubikira. Umekuwa  swafi.

7.  NI  ISHARA  KWAMBA  PESA  ULIYO  IPATA  HIVI  KARIBUNI  ITAISHA  YOTE  BILA  WEWE  KUFANYA  KITU  CHOCHOTE  CHA  MAANA :  Kama  umepata  pesa  nyingi  hivi karibuni  baada  ya  kusota  kwa  muda  mrefu  labda  kupitia  kilimo  au uchimbaji  madini  halafu  ukaanza  kuota  ndoto  umerudi utotoni  au  shuleni  basi  kuwa  makini  sana  na  matumizi  ya  pesa  zako  kwani  hiyo  ni  ishara  kwamba  pesa  zako  zitaisha  zote  hivi  karibuni  bila  wewe  kufanya jambo  lolote  la  maana. 

 Malaika  walinzi  wako  kwa  sababu  wana  uwezo  wa  kusoma  na  kuona  mambo  yatakayo  kutokea  katika siku  za  usoni, wanakupa  tahadhari  kwa njia  ya  ndoto. Kama  upo  katika  kundi  hili  hakikisha  unafanya  mambo  yote  ya  msingi  uliyo  kusudia  kuyafanya  hapo  mwanzoni  endapo  ungepata  pesa  ulizo  zipata. 

Kama  ulipanga  kununua, nyumba, ardhi, kufungua  kampuni, nakadhalika  basi fanya  hivyo  haraka sana  kwani  pesa zako zitaisha  zote  bila  kufanya  jambo  la  maana. 

Mara  nyingi  ndoto  hii  huwatokea  wale  wanao  pata  pesa  nyingi  na  kuingia  kwenye  maisha  ya  starehe  pamoja  na  wale  wanao pata  pesa  nyingi  halafu  wana  iacha  tu benki huku  wakisubiri  wapate  pesa  nyingine Zaidi  ndio wafanye  wanacho  taka  kukifanya.  

Sasa  hapa  Malaika  walinzi  wako  ambao  wana  uwezo  kuona  mambo  yatakayo  kutokea  mbeleni  wanajua  kuwa  pesa  hiyo  unayo  itaka  hutoipata  leo  wala  kesho. 

Itachukua  muda  mrefu  sana. Kwa hiyo  wanakutahadharisha  kuwa  pesa  yako  uliyo  weka  utaishia  kuitumia  kidogo  kidogo  hadi  itaisha  yote  hivyo  basi  kama  ulikuwa  na  biashara  unataka  kufanya  basi  anza  kufanya  sasa  kwa  pesa  hiyo  hiyo  uliyo  nayo.

8.TAFSIRI  NAMBA  NANE :  UNA TAHADHARISHWA  KUTOWEKEZA  PESA  ZAKO  KWENYE  BIASHARA  MPYA  AMBAYO  UNATAKA  KUIFANYA.

Umetoa  pesa  ya  mtaji  kutoka  kwenye  biashara  yako  moja  na  unataka  kuiweka  yote au  karibu  yote  kwenye  biashara  nyingine  halafu  ukaona  unaanza  kuota  ndoto upo  shuleni  au umerudi  utotoni  basi  tafsiri  yake  ni  kwamba,  endapo  utawekeza  pesa  zako  kwenye  biashara  hiyo  mpya  basi  pesa  zako  zitapotea  kwani  biashara  hiyo  haitokulipa.  

Ukiwa  katika  kundi  hili  na  ukawa  unaota  ndoto  hizo, nakushauri  ufanye  mambo  yafuatayo : Moja usiweke  pesa  zako  kwenye  biashara hiyo  kabisa, endelea  kufanya  biashara  yako  ambayo  umeizoea au  kwenye  hiyo  biashara  mpya  weka  pesa  kidogo  sana  ambayo  hata  kama  itapotea  basi  wewe  huto ijutia  sana.

9.TAFSIRI  NAMBA  TISA: NI ISHARA  KWAMBA  MPANGO  UNAO  TAKA  KUUFANYA  UTA KUSABABISHIA  HASARA  KUBWA  SANA  NA  UTAKURUDISHA  NYUMA  SANA.

Kama kuna  mpango  wowote  ambao  unataka  kuufanya  halafu  ukaanza  kuota  ndoto upo shuleni  au utotoni  basi  hiyo  ni  ishara  kwamba, mpango  huo  ambao  unataka  kuufanya  utakuletea  hasara  kubwa  sana  katika  maisha  yako  na  kukurudisha  nyuma  sana  kifedha  na  kimaisha.  Mpango unaweza  kuwa  wowote, mfano  kuacha  kazi  unayo  ifanya  na  kufanya  kitu  kingine, kuoa, kumroga  mtu  nakadhalika.

11. KWA  MTU  ALIE  BWETEKA  NA    KAZI  AU  SHUGHULI  ANAYO  IFANYA.

Anaweza kuota  ndoto  kama  ishara  kwamba kubweteka/kuridhika  kwake  kunamkwamisha  na  kumrudisha  nyuma  kimaisha na  kimaendeleo.

12. NI  ISHARA  KWAMBA  MUNGU  AMEKUFANYIA/ATAKUFANYIA  WEPESI KWENYE  JAMBO  UNALO  MUOMBA

Kama upo  kwenye  kipindi  kigumu  cha  maisha  na una muomba  Mwenyezi  Mungu  akufanyie  wepesi  kuhusu  magumu  unayo  yapitia  halafu  ukaota  ndoto  umerudi  utotoni basi  tafsiri  yake  ni  kwamba  Mungu  amejibu  maombi  na  dua  zako  na kwamba  mambo  yako  yatakuwa  mepesi  muda  si  mrefu.  

Mtoto  ni  kiumbe  ambae  maisha  yake  ni  mepesi  kwa  sababu  kila  kitu  anapata  kutoka  kwa wazazi  ama walezi  wake. Kwa  hiyo  kama  upo  kwenye  kundi  hili  basi  shukuru  kwa sababu  mambo  yako yanaenda  kufanyiwa  wepesi.

13.  NI  ISHARA  KWAMBA  TABIA  YAKO  YA  UZINZI  NA  UASHERATI  INAKURUDISHA  NYUMA   KIMAENDELEO

Hakuna  tendo  linalo  chafua  na  kuharibu  nyota  ya  mtu  kama uzinzi  na  uasherati. Nyota  ya  mtu  ikichafuka  na kuharibika  basi  na  mambo  yake  yatachafuka  na  kuharibika  pia.  Kama  unajihusisha  na  uzinzi  na  uasherati  halafu  ukaota  ndoto  umerudi  utotoni  basi  huo  ni ujumbe  kwamba, tabia  yako  ya  uzinzi  na  uasherati  inachafua  na  kuharibu  nyota  yako  na  inakurudisha  nyuma  kimaendeleo.  Kwa  hiyo  unatakiwa  kubadili  mwenendo  wako  haraka  iwezekanavyo.

14. NI  ISHARA  KWAMBA  KUNA  WATU  WANA IBA  MALI ZAKO  AU  MALI  ZAKO  ZINA  TEKETEA.

Kwa mfano  una  miliki  duka  au  maduka  na  kwenye  duka  au  maduka  yako umeweka  wafanyakazi  wa  kusimamia  duka  lako.  Ukiota  ndoto  umerudi  utotoni basi  ni  ishara  kwamba  kuna  watu  wanakuibia  mali  za duka  lako  na  hivyo  kukurudisha  nyuma.  Mfano  mwingine  ni  kama  una  lima  mashamba  au  unafuga mifugo  halafu  ukaota  ndoto  hii  ya  utotoni  basi jua  kuna  watu  wanakufanyia  hujuma  kwenye  mashamba  yako  au  mifugo  yako, hujuma  ambazo  zinakurudisha  nyuma  kimaendeleo.

Mfano  mwingine  ni  kama  upo  nje  ya  nchi  unayo  ishi  halafu  unatuma  pesa  kwa  ndugu, jamaa  au  rafiki zako waliopo  nchini  kwako  kwa  ajili  ya  kujenga  nyumba yako  na  kuisimamia, kununua  mashamba, mifugo  nakadhalika  halafu  ukawa  unaota  ndoto  ya  utotoni  basi  ni  ishara  kwamba nyumba  yako  haijengwi  na  ulio wapa  kazi  hiyo  wanakula  pesa  yako  tu.

17. KWA  MTU ALIYE  LISHWA  LIMBWATA  KWA  LENGO  LA  KUCHUNWA  PESA  NA  MALI  ZAKE : Anaweza  kuwa  anaota  ndoto  amerudi  shuleni  au  utotoni  ikiwa  ni  ishara  ya  kwamba  anarudishwa  nyuma  kimaisha  na  mtu  ambae  amemlisha  limbwata la  mapenzi.


Tafsiri zipo nyingi  sana  lakini  kwa  leo  hizi  zinatosha.

KUOTA   NDOTO UNAFANYA   MTIHANI   AMBAO  ULISHA  UFANYAGA  MIAKA  MINGI  IMEPITA .

Ndoto  hii  ni  tofauti  na  kuota  ndoto  umerudi shuleni. Ndoto  hii  ni tofauti kabisa  na  kuota  ndoto  umerudi  shule.

Ndoto hii  ina  maana  ifuatayo :  MAANA  YA  NDOTO  HII NI  KWAMBA  MTIHANI  WA  KIMAISHA  ULIO  PEWA, UMEUSHINDWA, KWA  HIYO  LAZIMA  UUFANYE  TENA  MTIHANI  HUO.  Na  usipo  ufanya  basi  utaendelea  kukuandama  katika  siku  zote  za  maisha  yako.

Kwa mfano wewe  ni  mwanaume, uliingia  kwenye  ndoa  halafu  baadae  ukagundua  kwamba  mke  wako  ni  mkorofi na sababu  hiyo  basi  ukaamua  kuachana  nae na  sasa  unatafuta  mwanamke  mwingine  ambae  sio  mkorofi.

Usicho  kijua  ni  kwamba  mwanamke  huyo  unae  muona  mkorofi  aliletwa  kwako  kama  mtihani  ambao  ulitakiwa  kuufaulu.  Mungu  aliuleta  mtihani  huo  kwako  ili  ujifunze  jinsi  ya  kuishi  na  mke  mkorofi . Sasa wewe  mtihani  huo  umeufeli, umemfukuza  mkeo  kwa  sababu  mkorofi. Ni  sawa  na  kuacha  kuandika  majibu  ya  mtihani  kwenye  chumba  cha  mtihani  kwa  sababu  maswali magumu. Kitatokea  nini? Utafeli  mtihani  huo. Na  ukifeli  mtihani  wa  kiroho  lazima  uurudie. Hakuna  mjadala  katika  hilo.

Sasa  basi  ukiwa  katika  mchakato  wa kutafuta  mke  mwingine  ambae  sio  ‘mkorofi’ kama  huyo  ulie muacha, halafu  ukawa  unaota  upo shule  unafanya  mtihani  ambao  uliufanyaga  miaka  mingi  imepita  basi  jua  kuwa  una fahamishwa  kwamba, unapoteza  muda  wako  kujaribu  kufanya  mtihani  ambao  ulishaufeli  kwa  sababu  hata  kwenye  mtihani  huo  utaenda  kufeli  pia.  

Hii  ni  kwa wote  wanawake  kwa  wanaume.

Ndio  maana  wapo  watu   ambao  hawatulii  kwenye  ndoa  moja.  Ndani  ya  miaka  kumi  mtu  ana  ndoa  tatu  na  zote  wameachana  kwa  sababu  zinazo  fanana.

Mifano  ipo  mingi  sana  ila huu  wa  ndoa  ni  mfano ambao  unaweza  kueleweka  kwa urahisi.

Ni  matumaini  yangu  kuwa  sasa  umejua  ni  kwanini  unaota  ndoto  ukiwa  umerudi  utotoni, upo  shuleni  unasoma  au   unafanya  mtihani  ambao  ulisha  ufanya  miaka  mingi  imepita.

IMESIMULIWA  NA   Dokta  Mungwa  Kabili…………………………………0744 -  000  473.



from MPEKUZI

Comments