Uamuzi Kesi ya Freeman Mbowe na Wenzake Kutolewa Leo


Leo Jumanne Desemba 14, 2021 Jaji Joachim Tiganga wa Mahakama ya Kuu, Divisheni ya Makosa ya Makosa ya Rushwa na Uhujumu Uchumi, anatarajia kutoa uamuzi katika kesi ndogo ndani ya kesi ya msingi kutokana na upande wa utetezi kuweka pingamizi kuhusiana na malezo ya onyo ya mshtakiwa wa tatu katika kesi hiyo, Mohamed Ling'wenya.

Mawakili hao wa upande wa utetezi walipinga maelezo hayo yaliyotolewa na SP Jumanne yasipokelewe na mahakama kwa sababu mshtakiwa huyo alilazimishwa kusaini na wala hajawahi kufikishwa kituo Kikuu cha Polisi Dar es Salaam.

Tayari washtakiwa tayari wameshafikishwa mahakamani kwa ajili ya kuendelea na kesi hiyo.  

Pia, awakili wa pande zote mbili nao wameshafika katika Mahakama kwa ajili ya kusikiliza uamuzi katika kesi ndiogo ndani ya kesi ya msingi.


from MPEKUZI

Comments