Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira Athibitisha Kuambukizwa Ugonjwa wa Corona

Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira ametangaza kuwa ameambukizwa virusi vya corona vinavyosababisha homa ya COVID-19.

Kiongozi huyo amesema, hafahamu ameambukizwa lini virusi hivyo na kwamba aliamua kupima kwa sababu kazi anazofanya zinahusisha muingiliano mkubwa na watu.

“Nimepima na matokeo yamekuja yameonesha nimeambukizwa virusi vya corona, sioni dalili za ugonjwa sina homa sikohoi lakini vipimo vimeonesha, hii ni dalili kwamba Watu wengi tunaweza kuwa tunetembea tukiamini tuko salama kumbe hatuko salama, sijui niliambukizwa lini “ – RC Mghwira


from MPEKUZI

Comments