Serikali Yatangaza Nafasi za Kazi 610 za Madaktari....Bofya Hapa Kujua Zaidi

Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Ofisi ya Rais - TAMISEMI) imepata kibali cha ajira ya Madaktari 610 watakaofanya kazi katika Mamlaka za Serikali za Mitaa nchini. 

Hivyo, Ofisi ya Rais - TAMISEMI inapenda kuwatangazia Madaktari wa Binadamu na Meno waliohitimu katika vyuo mbalimbali vya Elimu ya Juu vinavyotambulika na Serikali kuwasilisha maombi ya nafasi za ajira kuanzia leo tarehe 24/03/2020 ili kujaza nafasi mbalimbali katika Hospitali za Halmashauri na Vituo vya Afya kama ifuatavyo:-
 
1. Daktari Daraja la II /Daktari wa Meno Daraja la II (Nafasi 610)
 
Waombaji wawe na Shahada ya Udaktari wa Binadamu/Meno kutoka Vyuo Vikuu vinavyotambuliwa na Serikali waliomaliza mafunzo ya kazi kwa vitendo (Internship) kwa muda usiopungua mwaka mmoja na kupata usajili kutoka Baraza la Madaktari Tanganyika (Medical Council of Tanganyika).
 
SIFA ZA MWOMBAJI;
i. Awe raia wa Tanzania;
ii. Awe na umri usiozidi miaka 45;
iii. Awe na vyeti kamili vya mafunzo ya fani aliyosomea;
iv. Asiwe Mwajiriwa wa Serikali au asiwe Mwajiriwa wa Hospitali za Mashirika ya Dini ambaye mshahara wake unalipwa na Serikali;
v. Asiwe amewahi kuajiriwa Serikalini; na


from MPEKUZI

Comments