Algeria Yathibitisha Kuwa na Mgonjwa Wa Corona....Waliofariki Hadi Sasa Kwa Virusi Hivyo ni Watu 2,763

Algeria imethibitisha kisa cha kwanza cha virusi vya Corona, ambapo mgonjwa ni raia wa Italia aliyewasili nchini humo Februari 17. 

Tayari mgonjwa huyo amewekwa eneo maalumu la matibabu. 

Algeria inakuwa nchi ya pili ya Afrika kupata muathirika wa virusi hivyo baaada ya Misri.

Watu waliofariki  hadi sasa kwa virusi hivyo  Ulimwenguni wamefikia 2,763 huku Watu 80,970 wakiathirika
 

Wagonjwa 29,745 wamepona maambukizi hayo nchini China na kuruhusiwa kutoka hospitalini


from MPEKUZI

Comments