VIDEO: Maandamano ya kushinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania Iliyokamatwa Afrika Kusini yaanza Dar

Umati wa watu umejitokeza leo nje ya Ubalozi wa Afrika Kusini jijini Dar es Salaam ukishinikiza kuachiwa kwa ndege ya Air Tanzania iliyoshikiliwa nhini Afrika kusini kufuatia kesi ya fidia inayomhusu Bwana Hermanus Steyn wa nchi hiyo na Serikali ya Tanzania.

 
Ndege hiyo ya ATCL aina ya Airbus A220-300, ilizuiliwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Oliver Tambo jijini Johannesburg mwishoni mwa wiki iliyopita kwa amri ya Mahakama Kuu ya Gauteng nchini humo.

Baada ya ndege hiyo kushikiliwa, serikali ilituma jopo la wanasheria nchini Afrika Kusini likiongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Profesa Adelardus Kilangi kufuatilia suala hilo ili ndege hiyo iachiliwe haraka na kuendelea na safari zake kama kawaida. 




Video kwa hisani ya Azam tv


from MPEKUZI

Comments