Moto Wateketeza Ghala la Kiwanda Arusha

Moto  mkubwa ambao chanzo chake hakijajulikana, umezuka na kuteketeza moja kati ya maghala matatu ya kuhifadhia pamba katika kiwanda cha Sunflag kilichopo mkoani Arusha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Jonathan Shanna, amesema kuwa moto huo umeanza kuwaka kuanzia majira ya saa 7:00 mchana, ambapo hadi sasa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji limefanikiwa kuuzima moto huo.

“Bado hatujajua chanzo chake, maofisa wangu wanaendelea na uchunguzi,” amesema Shana


from MPEKUZI

Comments