Jeshi la Polisi Latoa Onyo Kwa Watakaofanya Vurugu Wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mtaa

Jeshi la Polisi nchini limewatahadharisha wale wote watakaoleta vurugu wakati wa uchaguzi wa Serikali za mitaa  na kusema watachukuliwa hatua kali za kisheria

Taarifa hiyo imetolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini David Misime, ambaye amesema kuwa watu wakifuata sheria chaguzi zote nchini zitabaki kuwa na amani.

“Wale ambao wanahisi watatingisha kiberiti kipindi cha uchaguzi wa serikali za mitaa, sisi tumejipanga vizuri kukabiliana nao kwa nguvu zote kwa jinsi ambayo tutazidi kupokea nguvu toka kwao au ubishani toka kwao” amesema Misime.


from MPEKUZI

Comments