Utomvu Ni Dhahabu Nyingine Inayopatikana Katika Shamba La Sao Hill.

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.
Watanzania kuanza kunufaika na zao la miti kutokana na uvunaji wa utomvu kutoka kwenye miti ya kupandwa iliyopo kwenye Shamba la Sao Hill lililopo Mufindi mkoani Iringa kwa kuiliingizia taifa zaidi ya shilingi bilioni mbili kwa kupindi cha miaka miwili ya majaribio.

Hiyo imebainika wakati wa ziara ya baadhi ya viongozi wa wilaya ya Chato,Mkoa wa Geita na viongozi wa vijiji vinavyolizunguka Shamba la Miti la Biharamulo lililopo mkoani Geita baada ya kutembelea Shamba la Miti Sao Hill linalosimamiwa na Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) kwa lengo la kujifunza shughuli mbalimbali za uendeshaji katika shamba hilo.

Akitoa ufafanuzi mkurugenzi wa Rasilimali Misitu na Nyuki TFS, Zawadi Mbwambo alisema kuwa Shamba la Miti Sao Hill wameanziasha mradi mpya wa kuvuna utomvu ambao umekuwa unatengenezewa gundi kwa ajili ya kutumika kwenye bidhaa mbalimbali kulinga na mahitaji ya wahusika.

“Tumeanza kugema utomvu kwenye miti mikubwa kwa kuwa tupo kwenye majaribia lakini wataalamu wamesema kuwa ukianza kugema utomvu mti ukiwa na umri mdogo basi utagemwa kwa muda mrefu na kuleta faida kwa wananchi na taifa kwa ujumla, na kumbukeni kuwa hapa mti haukatwe unaendelea kustawi tu” alisema Mbwambo

Mbwambo alisema kuwa takwimu za dunia zinaonyesha kuwa inawezekana utomvu ukawa unalipa zaidi ya zao la miti hivyo utafiti ukimalizika yawezekana wakulima wa miti wakahamia kwenye uvumaji wa utomvu.

“Kwa takwimu hizo sio muda faida kubwa itakuja kwa wananchi na serikali kwa ujumla maana inaonyesha dhahili kuwa utomvu unalipa sana kuliko mbao hiyo watafiti waliopo hapa katika shamba la Sao Hill ukizaa matunda basi utahamia kwa wakulima wa miti” alisema Mbwambo

Mbwambo alisema kuwa miti milioni tatu kila mwaka ndio inatumika katika uvunaji wa utomvu na hakuna eneo maalum ambao limetengwa kwa ajili ya kuvuna bali wametoa maeneo ambayo yanamiti ambayo inatarajiwa kuvunwa baada ya miaka miwili ijayo

“Shamba hili la Sao Hill ni kubwa sana linakaribia kuwa na hekta laki moja na elfu hamsini na nne hivyo sio rahisi kufanya majaribio shamba lote hiyo tumetoa eneo ambalo miti yake inatarajiwa kuvunwa baada ya miaka miwili” alisema Mbwambo

Mbwambo alisema kuwa soko la utomvu duniani kwa sasa linategemee kutoka nchi China hivyo soko lipo huko na kampuni ya AATY Limited ya kichini inavyovuna hapa katika shamba la Sao Hill na ni kampuni kubwa kuliko zote dunia za uvunaji wa utomvu duniani.

Akizungumza kwenye eneo la tukio mkuu wa msafara huo Mkuu wa Wilaya ya Chato Mhe. Eng. Mtemi Msafiri alisema kuwa wamejifunza kitu kipya ambacho hawakuwahi kukifikiria katika maisha yao kuwa uvunaji au ugemaji wa utomvu unalipa kwa namna hiyo.

“Navyo sema kuwa sasa tumegundua dhahabu ya kijani namaanisha hivi,utomvu unaigiza fedha nyingi tumeana hapa mkurugenzi katueleza hivyo ni lazima tuchukue swala hili kwa umuhimu stahili ili hata kweli kwetu Chato tutalifanya kwa umakini mno” alisema Msafiri

Shamba la Sao Hill lililopo hapa Mufindi lilianzishwa kwa majaribio mnamo mwaka 1939 hadi mwaka 1951 na upandaji kwa kiasi kikubwa ulianza rasmi mwaka 1960 hadi 1980 na shamba hilo linaukubwa wa hekta 135,903 ambazo zimehifadhiwa kwa ajili ya upandaji wa miti na uhifadhi wa mazingira na shamba hilo ni miongoni mwa mashamba 23 ya miti ya kupandwa ya serikali ambayo yanasimamiwa na wizara ya maliasili na utalii kupitia Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS).


from MPEKUZI

Comments