Polisi Watatu Akiwemo Staff Officer I Mkoa Wa Kipolisi Rufiji Wafariki Dunia

NA MWAMVUA MWINYI,MKURANGA
ASKARI wawili wa kanda maalum Rufiji, pamoja na staff officer I mkoa wa kipolisi Rufiji (ACP) ,Issah Bukuku ,wanadaiwa kufariki dunia katika ajali ya gari baada ya kupasuka gurudumu la nyuma na kupinduka na kusababisha majeruhi wawili.

Taarifa za awali kuhusu ajali hiyo zinaeleza,imetokea Julai 25 mwaka huu, huko kijiji cha Kilimahewa barabara ya Kilwa wilaya ya Mkuranga na mkoa wa kipolisi Rufiji ambapo gari namba PT. 3822 Toyota land cruiser mali ya jeshi la polisi mkoa wa kipolisi Rufiji likiendeshwa na askari namba F7167 PC Ibrahim likitokea polisi Ikwiriri kuelekea kijiji cha Mwalusembe wilaya ya Mkuranga .

Waliofariki dunia katika ajali hiyo ni staff officer I mkoa wa kipolisi Rufiji (ACP) ,Issah Bukuku ,inspector Esteria wa ofisi ya RCO Rufiji na G 1132 PC Lameck wa FFU Rufiji.

Majeruhi katika ajali ni dereva wa gari hiyo F 7167 PC Ibrahim wa ofisi ya RCO Rufiji ambaye ameumia sehemu mbalimbali za mwili wake na G7651 PC Mgusi wa ofisi ya RPC Rufiji ambaye ameumia sehemu mbalimbali za mwili wake.

Chanzo cha ajali ni kupasuka gurudumu la nyuma kulia na kusababisha gari hilo kupinduka.

Mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama wilaya ya Mkuranga, Filberto Sanga alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na taarifa kamili za kipolisi kanda maalum Rufiji zinaendelea na uchunguzi na itatoa habari kamili .


from MPEKUZI

Comments