Jamii Yatakiwa Kutowatenga Watu Wenye Ulemavu.

NA AVITUS BENEDICTO KYARUZI, KAGERA
Jamii mkoani Kagera imetakiwa kutowabagua wala kuwanyanyapaa  watoto wenye ulemavu  badala yake wapewe vipaumbele na  mahitaji  muhimu ili  wajione sawa na watu wengine. 

Kauli hiyo imetolewa  na mkuu wa taasisi ya Taasisi ya kuzuia na kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoani Kagera Bwana John Joseph wakati akiongea na Mwandishi wa kituo hiki ofisini kwake. 

Bwana Joseph amesema kuwa kuna baadhi ya watu ambao wamekuwa wakiwatenga, kuwabagua  watu wenye walemavu wakiwemo watoto jambo mbalo husababisha makundi hayo kujiona ni watu wa tofauti katika jamii 

 Amesema katika  ushiriki wa makundi ya vijana juu ya  mapambano dhidi ya Rushwa Taasisi  hiyo imefanikiwa kuyaelisha makundi ya wanafunzi kwa kuanzisha clabs za wapinga rushwa mashuleni 

Mkuu huyo amesema ili kulipa uzito suala hilo july 28 mwaka huu wanafunzi wa shule ya Sekondari Kahororo iliyoko mkoani Kagera  kwa kushirikiana na Taasisi hiyo watakwenda kutembelea  shule ya wanafunzi walemavu katika shule sekondari  Mgeza Mseto kwa ajili ya kuwapelekea mahitaji  mbali mbali mbali. 

Amesema  makundi ya watu wenye walemavu ni sehemu ya jamii na ili makundi hayo yatambue kuwa jamii haijawatenga kila mmoja ashiriki katika kuwatembelea kuwajali na kuwapa chochote walemavu waliopo katika maeneo yake. 

Hata hivyo ameongeza kuwa jamii iwafichuo na kuwaweka adharani wapate Elimu pamoja na mahitaji yao muhimu.


from MPEKUZI

Comments