Azim Dewji ,waandishi Watatu Wanusurika Ajalini

Mfanyabiashara, Azim Dewji, na waandishi watatu wa vituo vya televisheni vya ITV,  Channel Ten na Azam TV wamepata ajali jana, Julai 27, 2019, asubuhi baada ya gari lao kuacha njia wakati wakiwa njiani kuelekea Rufiji kwenye sherehe za uwekaji jiwe la msingi la mradi mkubwa wa umeme wa MW 2,115 wa Rufiji mkoani Pwani.

Kwa sasa Azim Dewji amelazwa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kitengo cha  mifupa (MOI) akipatiwa matibabu baada ya mfupa wake mmoja wa uti wa mgongo kuvunjika ajalini. Watu wote waliokuwa kwenye gari hilo wametoka salama.



from MPEKUZI

Comments