Waziri Mkuu: Kesho Ni Siku Ya Mapumziko

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema kesho tarehe 26 Aprili, 2019 ni siku ya mapumziko na hakutakuwa na shamrashamra za sherehe.

Akizungumza ofisini kwake jijini Dodoma leo (Alhamisi, Aprili 25, 2019), Waziri Mkuu amesema kesho ni siku ya mapumziko kitaifa kuadhimisha kumbukumbu ya miaka 55 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar lakini hakutakuwa na sherehe.

Amesema jumla ya sh. milioni 988.9 ambazo zilikuwa zimepangwa kwa ajili ya sherehe hizo, zimeokolewa na zitapangiwa shughuli nyingine.

(mwisho)

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,


from MPEKUZI

Comments