Mahakama: Ni Marufuku Kuchora Vibonzo Vya Kumkejeli Rais wa Rwanda

Mahakama Kuu nchini Rwanda imetupilia mbali mashtaka yaliyokuwa yametolewa na baadhi ya wanasheria nchini kupinga sheria iliyoanzishwa mwaka jana kuwa ni kosa la jinai kuchora vibonzo vinavyomkejeli Rais wa nchi hiyo.

Wanasheria hao walifungua kesi kulipinga hilo huku wakisema hiyo ilikuwa ni kinyume cha katiba ya nchi hiyo. 

Hata hivyo mahakama hiyo imeamua kuwa viongozi wengine waandamizi serikalini na viongozi wakuu wa kidini halitakuwa kosa la jinai kuwachora kwenye vibonzo.


from MPEKUZI

Comments