Jumuiya za watumia maji njombe zatakiwa kutunza mitandao ya maji

Na Amiri kilagalila Njombe
Halmashauri ya wilaya ya Njombe kwa kushirikiana na shirika la maendeleo la nyanda za juu kusini  SHIPO  imeadhimisha kilele cha wiki ya maji  kwa kutoa elimu kwa viongozi wa  jumuiya 22 za watumia maji  za wilaya hiyo ambazo pamoja na kupatiwa elimu ya utunzaji wa miundombinu ya maji na vyanzo pia zimetembelea jumuiya kubwa ya watumia maji ya Tove-Mtwango na kujifunza namana ya kusimamia jumuhia zao.

Wakizumza na mtandao huu  baadhi ya viongozi wa jumuiya za watumia maji kutoka wilayani njombe wamesema kuwa miradi mingi ya maji inakufa na kushindwa kuwa endelevu kutokana na gharama za uchangiaji matumizi ya maji kuwa chini hali inayasababisha miradi kushindwa kujiendesha.

“Kwa ujumla wenzetu wako juu sana tofauti na ninakotoka mimi hata kama mradi wao ni wa mtiririko inaonekana wao maji ni mengi na wenzetu wana kamati ambazo zimekamilika na kila wakati wana vikao namna ya kuendesha huu mradi na kwa ufupi kulingana na vikao wanavyoviweka basi ndivyo maendeleo yao ya uendeshaji wa maji yanavyofanikiwa” alisema TULAWONANA MANGI’TA mwenyekiti wa jumuiya ya watumia maji Ikuna

Kaimu mhandisi wa maji halmashauri ya wilaya ya Njombe Kinganola sanga na Olaisi ole Mgaya mratibu wa miradi ya maji kutoka shirika la shipo wamesema lengo la kufanya ziara katika mradi huo wa tove mtwango ni kutaka viongozi hao wajifunze namna ya  kuendesha  jumuiya katika maeneo yao kwa ubora wa hali ya juu.

“Tumekutana kwa lengo la kuelimishana na kukumbushana Tove mtwango ni jumuiya inayosifika na inafanya vizuri na inatekeleza mradi kwa zaidi ya vijiji 16 vya wilaya ya Njombe na Wanging’ombe  na kwa sababu hiyo ni sehemu nzuri kwa jumuiya zingine kujifunza namna wenzao wanavyo tunza na kulinda mitandao ya maji ili iwe endelevu kwa vizazi vya sasa na vijavyo”walisema KINGANOLA SANGA na OLAISI OLE MNGAYA mratibu wa miradi ya maji Shipo.

Jumuiya ya watumia maji ya Tove- Mtwango ina vijiji 16 na iliasisiwa tangu mwaka 2008 baada ya mradi huo wa maji  kukamilika uliojengwa  kwa ufadhili wa kanisa katoriki kwa kushirikiana na  serikali ambapo jumuiya hiyo imetajwa kuwa na  mipango mizuri ya usimamizi.

“Kwa kweli tumejipanga sasa kuhakikisha tunafunga mita kwa ajili ya vituo vyetu vya maji kwa sababu havina maji na tutafanya hivi ili kuhakikisha hakuna tone lolote la maji litakalopotea”alisema ABDALA MTEMI meneja wa jumuiya ya watumia maji Tove mtango.


from MPEKUZI

Comments