Askari Magereza Ajiua kwa Kujipiga Risasi Kidevuni

Askari Magereza katika Gereza la Kilimo Kitai wilayani Mbinga, Ruvuma, Adamu Kulwa Mgaga (24), amejiua kwa kujipiga risasi.
 
Askari hiyo mwenye namba B:8400 WDR, amejiua akiwa lindo la mifigo kwa kujipiga risasi eneo la kidevu na kusababisha kichwa kupasuka
 
Mkuu wa Magereza Mkoa wa Ruvuma, Arekizanda Nyifwa, alithibitisha kutokea kwa tuko hilo Desemba 25, mwaka huu, saa 2:30 usiku katika gereza la Kitai-Mbinga.
 
Alisema askari huyo alipokuwa lindo ilipofika saa 2:30 usiku alichukua bunduki aliyokuwanayo aina ya SAR na kuelekeza bomba kwenye kidevu chake kisha kuhesabu moja hadi tatu na kufyatu risasi ambazo zilifumua kichwa chake na kufariki dunia papo hapo. 

Alisema askari huyo alifanya hivyo akiwa katika sare za jeshi hilo na kwamba chanzo cha kujiua bado hakijafahamika kwa kuwa hakuacha ujumbe wowote.Alisema polisi wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo.


from MPEKUZI

Comments