Makamu wa Rais: Msichague Viongozi Mazezeta Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa 2019

Na Mwamvua Mwinyi,kibaha
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Samia Suluhu amewataka wananchi wa Kibaha Mjini Mkoani Pwani ,wajipange kuchagua viongozi wepesi kufuatilia maendeleo na kwenda mbio badala ya kuchagua mazezeta na mananga ,katika uchaguzi unaokuja wa serikali za mitaa- 2019.
 
Akihitimisha ziara yake ya siku sita mkoani hapo katika mkutano wa hadhara ,Mailmoja Samia aliwasihi wasichague watu wazito,wezi na mafisadi bali waweke viongozi watakaojenga Kibaha .
 
“Wanasema mjenga nchi ni mwananchi mwenyewe ,mimi nikija ninaona kasoro zilizopo nitakwambieni kuna kasoro lakini warekebishaji ni nyinyi na viongozi mtakaowachagua “;:
 
“Mkichagua wazuri wataondosha kasoro zilizopo haraka lakini mkichagua wazito na mananga hapa yatazama tuu chini kunyanyuka hayanyanyuki ,kutembea hayatembei “alisisitiza Samia .
 
Akizungumzia suala la ardhi anasema”:; Wakati napita ,mheshimiwa mkuu wa mkoa alinionyesha eneo kubwa halina kitu chochote nikamwambia mnataka manispaa ,lakini mbona eneo hili mwitu mtupu hakuna kuendelezwa akaniambia linamilikiwa na taasisi fulani “
 
Aidha ,ameitaka wilaya na halmashauri ya Mji huo kukaa chini na taasisi ambazo zimehodhi maeneo bila kuyaendeleza katika kipindi kirefu ili ziweze kuingia ubia  .
 
Awali Mbunge wa jimbo la Kibaha Mjini ,Silvestry Koka aliomba mji huo upandishwe hadhi na kuwa manispaa kama vigezo vinaruhusu.
 
Alitaja changamoto zinazowakabili kuwa ni ,usambazaji wa maji kwenda kwa wananchi unasuasua kasi iongezwe kwani mji unakua ila maji hayajawafikia .
 
” Eneo la Tamco-Mapinga zaidi ya miaka mitano wapo wananchi walifanyiwa tathmini lakini hawajalipwa fidia zao ,tunaomba utusaidie wananchi hawa waweze kufaidika na fidia hizo”alielezea Koka.
 
Koka alitaja tatizo jingine ni ucheleweshaji wa nishati ya umeme , kasi ni ndogo kufika kwa baadhi ya maeneo na wawekezaji ,ameomba uwafikie maeneo yaliyo katika miradi mbalimbali inayoendelea kutekelezwa.
 
Akijibu changamoto hiyo, Naibu waziri wa nishati ,Subira Mgalu alisema , kupitia serikali ipo sheria iliyoanzisha wakala wa nishati ya umeme vijijini lakini maeneo ya miji sheria ile ilikuwa huwezi kufanya miradi ya umeme mijini.
 
“Serikali ya awamu ya tano kwa makusudi mazima iliona miji ifaidike na raslimali zinazopatikana kwenye mfuko wa umeme vijijini na kwa maelekezo yenu tulibuni mradi wa Peri Urban”;alifafanua Subira.
 
Subira alisema ,kiasi cha sh. bilioni 82 zimetengwa kwa ajili ya mradi huo na sasa hatua iliyopo ni kumpata mkandarasi ili mradi uanze kazi .
 
Aliwahakikishia wananchi ambao hawana umeme katika kata ya Mailmoja ,Viziwaziwa,Pichandege ,Pangani, Misugusugu ,Sofu watanufaika na mradi huo .
 
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ramadhani Maneno, alisema Pwani ipo salama na ushindi ni lazima ,iwe jua iwe mvua uchaguzi ujao wa serikali za mitaa atahakikisha wanashinda


from MPEKUZI

Comments