Hanspope afikishwa Mahakamani Leo

Mwenyekiti wa kamati ya Usajili ya klabu ya Simba, Zacharia Hans Poppe na mfanyabiashara Franklin Lauwo wamefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Jumanne Oktoba 16, 2018 .

Hans Poppe na Lauwo baada ya kufikishwa mahakamani hapo wamepelekwa moja kwa moja katika chumba cha mahabusu wakisubiri kupandishwa kizimbani.


Mwenyekiti huyo wa usajili wa Simba amefikishwa mahakamani hapo siku moja baada ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) kukiri kumkamata Airport akitokea Dubai.


April 2018, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) ilitangaza dau nono la Shilingi Milioni 10 kwa yeyote atakayefanikisha kukamatwa kwa mfanyabiashara huyo na mwenzake Frank Lauwo.


from MPEKUZI

Comments