Mrembo kutokea Rwanda alikana Penzi la Diamond

Mrembo kutokea nchini Rwanda, Shaddy Boo amefunguka iwapo amewahi kutoka kimapenzi na Diamond Platnumz.

Jana kwenye Red Carpet ya Biko Jibebe Challenge, Shaddy Boo akizungumza na Waandishi wa Habari alijibu hilo kwa kueleza kuwa yeye na Diamond ni marafiki tu.

"Nothing is much, we just are friend yeah!, aah!, no!, is not true we are friend," alisema Shaddy Boo.

Mara kadhaa Diamond alipoenda nchini Rwanda amekuwa akionekana naye na kuna kipindi ilielezwa walikuwa wote nchini Kenya. 

Pia mrembo huyo amekuwa akionekana akiimba na kucheza zaidi nyimbo za Diamond kupitia ukurasa wake wa Instagram.


from MPEKUZI

Comments