Kagere aitosa rasmi Yanga

Na, magdalena kashindye
Mshambiliaji wa timu ya Gor mahia ya Kenya na raia wa Rwanda meddie kagere amesaini mkataba wa kuitumikia simba kwa miaka miwili.

Nyota huyo anayejua kucheka na nyavu amemalizana na wekundu wa msimbazi simba kuitumikia timu hiyo kwa kandarasi ya miaka miwili kwa thamani ya shilingi milioni 110 za kitanzania.

Mshambiliaji huyo aliyekuwa akiwindwa na timu ya yanga atakuwa ameitosa rasmi  timu hiyo iliyokuwa inamuwinda kuongeza nguvu katika mchuano ya kimataifa .

Timu ya Gor mahia tayari imeziba pengo la kagere kwa kumchukua Mshambiliaji wa kimataifa wa Uganda anayechezea vipers FC Eris Ssekisamba.


from MPEKUZI

Comments