Brazil Yatinga 16 Bora Kombe La Dunia,yaichapa Serbia 2-0

Baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Serbia, sasa Brazil imevuka katika hatua ya makundi na kwenda mtoano.

Hatua ya 16 ni hatua ya kwanza ya mtoano katika Kombe la Dunia na Brazil itakutana na wapinzani wao Mexico huku walioshika nafasi ya pili katika kundi lao, Switzerland wakikutana na Sweden.

Brazil, imeonyesha kuwa inakwenda inaimarika lakini bado vijana wengi washambulizi kama Gabriel Jesus, Willian, Neymar na wengine hawajaonyesha cheche zilizokuwa zikitarajiwa.


from MPEKUZI

Comments