Waziri Mkuu Amuwaklisha Raisi John Magufuli Katika Mkutano Wa AU Rwanda

Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa leo amemwakilisha Rais John Magufuli katika sherehe za kusaini mkataba wa kulifanya Bara la Afrika kuwa eneo huru la biashara jijini Kigali, Rwanda.

Tanzania ni miongoni mwa nchi zaidi ya 50 ziilizosaini mkataba huo, ambao umeelezwa utaongeza chachu kwa Afrika kuimarika kiuchumi.

Mkataba huo umesainiwa baada ya kukamilika kwa kamati za wataalamu zilizoshirikisha pia mawaziri wa biashara na mambo ya nje wa nchi washirika.

Mbali na mkataba huo, marais hao pamoja na wawakilishi wa nchi washirika wamesaini Itifaki ya utekelezaji wa makubaliano hayo ambayo yanatoa uhuru wa makazi, kutembea, haki ya kuishi na kufanyakazi popote Afika bila vikwazo wala vizuizi sambamba na Tamko la Kigali.

Sherehe hizo pia zimehudhuriwa na Mwenyekiti wa Makampuni ya IPP, Reginald Mengi na Mwenyekiti wa CEO Round Table, Ally Mufuruki ambaye jana alikuwa miongoni mwa wazungumzaji katika mjadala wa uchumi na biashara.


from MPEKUZI

Comments