Rais Magufuli Alivyotatua Kero ya Mizigo wa Mmiliki kiwanda cha mvinyo Papo kwa Papo!

Rais John Magufuli ameagiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuruhusu chupa za mvinyo zilizozuiliwa bandarini kwa  sintofahamu ya masuala ya kodi

Akizungumza leo Jumatatu Machi 19, Rais Magufuli ameitaka TRA kumpa mmiliki wa kiwanda cha mvinyo cha Dodoma chupa zake kwa kodi ya bei iliyoinunulia.

“Haya TRA mpeni chupa zake za mvinyo kwa kutoza kodi ile anayodai amenunulia chupa hizo,” ameagiza.

Akiwasilisha kero hiyo, mwakilishi wa kiwanda hicho aliyejitambulisha kwa jina moja la Minde, amesema chupa zake zimekwama bandarini kwa sababu anadaiwa kodi kubwa kuliko uhalisia wa aliyonunulia bidhaa hiyo.

Amesema ingawa amewaonyesha risiti lakini wamekataa kumpa mzigo huo, kwa sababu kodi anayodaiwa ni kubwa.


from MPEKUZI

Comments