Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) yatahadharisha mvua kubwa mikoa 11

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya vipindi vya mvua kubwa vinavyotarajiwa kuendelea katika maeneo ya mikoa 11 nchini.

TMA imetaja mikoa itakayoathirika na mvua hizo ni Dar es Salaam, Pwani, Lindi, Mtwara, Morogoro, Ruvuma, Rukwa, Mbeya, Songwe, Iringa na Njombe.

Taarifa iliyotolewa leo na mamlaka hiyo inabainisha kuwa kuanzia leo Machi 12 hadi 13 ,2018 kunatarajiwa vipindi vya mvua kubwa inayozidi milimita 50 ndani ya saa 24.

“Hali hii inatokana na kuendelea kuimarika kwa ukanda wa mvua, wakazi wa maeneo yaliyotajwa wanatakiwa kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa na tahadhari zinazotolewa, TMA inaendelea kufuatilia hali hii na itatoa mrejesho kila itakapobidi,” imesema sehemu ya taarifa hiyo.


from MPEKUZI

Comments