Diamond Kamjibu Tena Naibu Waziri wa Habari......“Unalijua leo baada ya kukosa point sahihi?”

Baada ya Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Juliana Shonza kukataa kumjibu Diamond, msanii huyo ameibuka tena yakiwa ni masaa takribani 23 yamepita tangu alipomjia juu kupitia kipindi cha The Playlist.

Diamond ameonekana kukerwa na majibu ya Naibu Waziri Shonza ambayo amekuwa akiyatoa kuhusu kufungia nyimbo za wasanii bila ya kuwapa taarifa sahihi na kuamua kumjibu kwa mara nyingine na safari hii ametumia mtandao wa Twitter.

Kupitia mtandao wa huo Diamond ameandika:
Swala la Barua Unalijua leo baada ya Kukosa Point sahihi? Ungekuwa unajua kama taratibu sahihi ni Kuandika Barua, Mbona hukuwatumia pia Wasanii barua zakuwa unafungia kazi zao?… kwakuwa Uliyapeleka Social Media na Radio, nami nikakupelekea huko ili uenjoy Zaidi…❤



from MPEKUZI

Comments