AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 39 na 40 )

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA 

Dada huyo mwenye weusi wa maji ya kunde, akaanza kuminya batani za kompyuta yake, alipo maliza, akanitingishia kichwa na kuniambia kwamba pesa tayari imesha ingizwa kwenye akaunti yangu. Gafla tukasikia mlio wa risasi ulio tufanya watu wote ndani ya benki kuhamaki, nikageuza macho yangu mlangoni nikamuona askari mmoja akiwa amenguka chini damu zikimwagika, huku majambazi sita wakiingia ndani ya benki wakiwa na bunduki pamoja na mabomu ya kurusha kwa mkono na mmoja kati ya majambazi hawa ni mwanamke na yeye ndio anaye ongoza msafara wa majambazi wezake huku mkononi mwake akiwa ameshika bunduki aina ya AK 47, bila hata ya kuhofia akapiga risasi mbili hewani na kufanya watu wote kulala chini hadi mimi mwenywe.

ENDELEA
Kila mmoja aliyopo kwenye eneo hili hususani ndani ya hii benki, mwili wake uliweza kutetemeka kwa woga, hapakuwa na mtu ambaye anapenda kufa kwa muda huu, hususani mimi ambaye ni masaa machache tu nimetoka kupewa zawadi nono kutoka kwa raisi wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
“Toa pesa wewe malaya”
Aliongea jambazi mmoja wa kiume huku akipapasa, watu waliokuwa wapepanga foleni ya kueleka katika dirisha la kuweka pesa au kutoa pesa. Jasho likazidi kunimwagika. Mtoto wa kiume ujanga sikuwa nao kusema kweli, japo nina mafunzo tosha ya kupambana na majambazi kama hawa ila hakuna kitu kibaya kwa mwanausalama yoyote dunia, kuwahiwa kushambuliwa, wenyewe kwa lugha yetu tunaita Ambushi.
Nikatazama jinsi watu wakipapaswa huku majambazi wengine wakiwashika wahudumu wa benki na kuingia nao kwenye vyumba ili waonyeshwe pesaa.

‘Natakiwa kufanya kitu’
Nilizungumza kimoyo moyo huku nikitazama majambazi hawa kwa umakini japo kichwa changu nimekilaza chini na mikono yangu nimeiweka kichani ila usawa wa macho yangu ulinitosha kuweza kuoana jinsi majambazi hawa walivyo simama huku wengine wakiendelea na shuhuli ya kutafuta pesa zilipo wekwa. Nikamuona jambazi mmoja akimfwata dada aliye kuwa ananihudumia, akamtandika kofi zito la shavu.
“Toa pesa wewee”
“S..si….si….na mimi”
Jambazi huyo akamtandika, kitako cha buduki cha tumbo na kumfanya dada hyo kuanguka chini na kutoa mlio mkali wa maumivi.
“Nyamaza wewe malaya nitakuchangua ubongo”
Kauli ya jambazi huyo ilinizidi kunitisha, kwani bunduki yake amemuelekezea dada huyo huku akiwa ameikoki vizuri tauyari kwa kufyatua risasi.
‘Unapo kuwa peke yako kwenye uvamizi, mfano uvamizi wa benki, super makert na kadhalika, hakikisha kwamba unamuwahi kiongozi wa hilo tukio, ukimpata tu huyo wezake hawato weza kufanya chohcote dhidi yako’

Maneno hayo ya mwalimu  wangu yakajirudia kichwani mwangu kwa kasi ya ajabu na kunipa ujasiri wa haraka ulio nifanya, nimtafute mkuu wao ambaye ni mwanamke, nikamuona akimpitia mtu mmoja baada ya mwingine akimgonga gonga kwa mguu na kutazama kama ana silaha au laa. Taratibu akazidi kunisogelea mimi, na mimi nikajiweka tayari kufanya shambuli la haraka sana kwa maana nina hapa nilipo nina silaha za kutosha. Kitendo cha kunikaribi, ikawa ni moja ya kosa kubwa kwake, kwani kwa sekunde moja niliweza kujigeuza na kurusha teka lililo izoa miguu yake na kuanguka chini huku bunduki yaki ikiwa pembeni, nikampiga kabali, na kunyanyuka naye, na kuwafanya wezake zote kusitisha kile walisho kuwa wakikifanya.

“Wote silaha zenu wekini chini”
Nilizungumza kwa kufuko huku bastola niliyo kuwa nimeiweka kiunoni nikiwaelekezea bosi wao kichwani. Majambazi wakabaki wakiwa wameduwaa, nikarudia tena kwa ukali kwamba waweke silaha zao chini lasivyo nina mwaga ubongo mwenzao huyu. Dada huyu akatoa ishara ya vidole akiwaamrisha waweke silaha zao chini, kila mmoja akafanya hivyo.
“Dany unafanya nini?”
Sauti ya dada huyu ikanistua sana kwa mana ni sauti ya mtu ambaye ninamjua vizuri tena vizuri sana.
“ASAMA………!!!”
Nikataka kumvua kinyago alicho kivaa usoni mwake, ila nikastukia kitu chanye ncha kali kikizama kwenye mbavu zangu za kushoto na kujikuta nikimuachia Asma na mimi nikidondoka chini, hapo ndipo nikaona kisu alicho nichoma nacho kikivuja damu huku kikiwa kiganjani mwake. Majambazi wezak wakaokota bunduki zao kwa haraka. Mmoja wao akataka kunipiga risasi, ila Asma akamzuia kwa haraka.



from MPEKUZI

Comments