SORRY MADAM -Sehemu ya 100 na ya MWISHO (Destination of my enemies)

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA  

“Shitiii”
Agnes akaikoki bunduki yake na kumuelekezea mtu huyo na kumpima maeneo ya kichwa. Mzee Godwin hadi anakaribiana na Erickson akaweza kuona alama nyekundu ya buduki ikiwa imemlenga Erickson kifuani. Kwa haraka Mzee Godwin akamuwahi Erickson ambaye anatambua ni mkwe kwa mwanaye Manka, akamsukuma na risasi ambayo ilipangwa kumpiga Erickson ikapiga mzee Godwin mgongoni na kumuangusha chini na kumfanya Eddy kushangaa na kwaharaka akaipiga magoti chini na kumgeuza Mzee Godwin na kumkuta akimwagikwa na damu mdomoni.
“BABABAAAAAAAAAA”
Eddy alipiga kelele humu machozi yakianza kumwagika usoni mwake na kumfanya Mzee Godwin kutabasamu na kumshika mkono wa kulia Eddy na kuuweka kifuani mwake.

ENDELEA
“Eddy”
Mzee Godwin aliweza kuitambua sauti ya Eddy na kulia kwake. Eddy kwa hasira akaanza kuivua sura yake ya bandia, japo imeshikana sana na ngozi ya uso wake, ila hakujali hayo maumivu.  Mzee Godwin akaendelea kumuangalia Eddy kitu anacho kifanya hafi ikafikia hatua akamaliza kabisa kuivua sura yake na kubaki na sura alisi.
“Baba fungua macho please”
Eddy alizungumza huku machozi yakimwagika usoni mwake. Japo baba yake huyo ameweza kumfanyia mambo mengi mauvu katika maisha yake yote ila damu ni nzito kuliko maji.
“Ku….uu…wa…..jasiri D.F.E1993”

Mzee Godwin alizungumza maneno hayo kwa shida kidogo na hapo hapo akakata roho. Kitendo cha mzee Godwin kuanguka chini na kunyanyuliwa na Erickson, kiliweza kumstua Manka aliye anza kushuka kwenye gari kwa garaka, na kuanza kukimbilia eneo alipo kaa Mzee Godwin na Erickson. Agnes hakutaka kumpa nafasi nyingine mlinzi wa John ambaye alikuwa akihangaika kuikoki bunduki yake. Akamtandika riasi moja ya kicha na kumchangua hapo hapo. Makachero wengine walipo ona makubaliano yameingia dosari wakaanza kufaya mashambulizi kwa kina Rahab na Fetty, ambao nao waliweza kuyajibu mashambulizi hayo huku wakiwa amejificha pembeni ya gari lao.
Agnes akashusha pumzi huku akimtazama Manka kwa kutumia lenzi ya bunduki yake, akikimbilia eneo alipo Erickso.

“Mpumbavu wewe”
Agnes alizungumza huku akiikoki bunduki, yake. Alipo hakikisha Manka amekaribia kufika karibu kabisa na walipo Eddy na mzee Erickson, akaivuta traiga ya bunduki hiyo na kuiruhusu risasi moja kutoka kwa kasi. Kitendo cha Manka kumtazama Erickson na kukuta akiwa ni Eddy, alistukia akianguka chini na hapo hapo akakata roho, risasi aliyo ifyatua Agnes iliweza kutua kichwani mwa Manka ndio iliyo yakatisha maisha ya msichana huyo.

Eddy alihisi kuchanganyikiwa, baada ya kumuona Manka akiwa amelala chini, damu nyingi zikiwa zimesambaa kwenye  lami. Halima na Anna wakiwa chini ya maji, waliweza kupambana na makachero wengine ambao walitumwa kuimarisha ulinzi chini ya daraja hilo. Mapambano yao yakawa ni kufa na kupona. Halima akajitahidi kupambana kadri ya uwezo wake, ila kwa leo bahati haikuwa kwake kwani kachero aliye kutana naye aliweza kumzidi kwa kila kitu na kujikuta akifia kwenye mikono ya kachero hiyo kwa kuchomwa kisu cha shingoni.

Kifo cha Halima, kilimshangaza sana Anna, aliye jikuta akiivunja shingo ya kachero aliye kuwa akipambana naye na kuimtoa mtungi wa gesi alio jifunga nao mgongoni. Akamfwata kachero aliye muua Halima, akaanza kuparanganaye, mapigano kati yao yaliweza kumpa ushindi Anna japo naye aliweza kujeruhiwa na kisu cha kachero hiyo ila akafanikiwa kummaliza maisha yake.

Taratibu Anna akaanza kuufwata mwili wa Halima sehemu unapo elea elea. Akaushika, na kujikuta akianza kulia kwa uchungu, kwa maana hakutarajia kama rafiki yake huyo anaweza kukutwa na mauti. Agnes kazi yake ikawa ni kuwaua makachero wote ambao wanapambana na kina Fetty na Halima. Haikuwa kazi ngumu kwake kwa maana sehemu alipo jificha ni si rahisi kwa mtu kuweza kumuona ila yeye aliweza kuona eneo zima.
                                                                                                       ***
    Wanajeshi na walinzi walio weza kubaki ikulu kwa ajili ya kuimarisha ulinzi kwa siku hiyo hawakuwa na bahati, kwa maana waliweza kushambuliwa na wanajeshi ambao wamevalia kombati za jeshi la taifa, ila utoafuti ni kwamba karibia wote wamejifunga vitambaa vyekundu katika mikono yao ya kushoto. Walijitahidi kuilinda Ikulu ila hawakuweza kwa maana shambulizi hilo ni kubwa na la kustukiza. Meja Paul Msuya aliweza kuwaongoza vijana wake katika kufanya mapinduzi hayo ya kuing’oa serikali yam zee Godwin madarakani.

   Zoezi lao halikuchukua muda mrefu sana, wakawa wamesha maliza kazi yao na kuiwek aikulu chini ya ulinzi wao. Meja Msuya akatuma wanajeshi wengine kwenda katika daraja la kigamboni kumsaidia mkuu wao ambaye ni Rahab. Milio ya risasi, iliwafanya wakazi wa maeno ya Posta na Kigamboni kuingiwa na hofu kubwa sana, kwa maana sio hali ya kawaida na hawakujua ni kitu gani kinacho endelea. Wananchi wengi walio ingiwa na woga, kila mmoja aliweza kujificha sehemu ambayo alihisi anaweza kuokoa maisha yao.

Wapo ambao waliweza kujificha chini ya vungu za vitanda vyao, wengine walijificha kwenye makabati, wengine waliamua kujifuanika mashuka gubigubi na kujinyoosha vitandani mwao na kuigiza kama wamekufa. Ukawa ni usiku mgumu sana kwao. Wanajeshi wanao muunga mkono Rahab, wakafika katika dareja la Kigamboni na kukuta mambo ndio yanamalizikia malizikia, huku walinzi wengi wa raisi Godwin wakiwa wamesha potea maisha yao. Wakaweza kuuona mwili wa mzee Godwin na mwanaye Manka wakiwa tayari wamesha teketea kwa kupigwa risasi.



from MPEKUZI

Comments