Serikali Yaridhia Gharama za Mazishi ya Akwilina....Yagoma Kutoa fedha taslim

Familia ya marehemu  Akwilina Akwiline inaendelea na maandalizi ya mazishi, huku ikielezwa kuwa Serikali imekubali kuyagharimia lakini si kutoa fedha.

Serikali imefikia hatua hiyo baada ya jana Februari 20,2018 familia ya Akwilina kueleza kuwa bajeti ya mazishi ni Sh80 milioni.

Katibu wa kamati ya mazishi Moi Kiyeyeu, ambaye ni kaka wa Akwilina amesema Serikali imewajibu kuwa haitawapa fedha taslim bali itagharimia vitu vilioorodheshwa katika bajeti ya mazishi hayo.

"Tulipotoa bajeti hatukuwa na maana kuishinikiza Serikali itoe fedha zote bali ilikuwa mahitaji ya msiba hadi pale utakapoisha. Tunashukuru Mungu kwa Serikali kuridhia kugharimia," amesema Kiyeyeu.

Kuhusu hilo, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia katika taarifa iliyotolewa leo Februari 21,2018  imesema kupitia kwa Katibu Mkuu wake, Dk Leonard Akwilapo ilipokea makisio ya gharama za mazishi ya Sh80 milioni kutoka kwa msemaji wa familia, Festo Kavishe.

Mkuu wa kitengo cha mawasiliano cha wizara hiyo, Mwasu Sware alisema baada ya kupokea makisio hayo Dk Akwilapo alitahadharisha kuwa kuna baadhi ya matumizi hayatakubaliwa kwa kuwa kisheria hayagharamiwi na Serikali.

Pia, katika makisio hayo kuna gharama ambazo zilikuwa zimepewa makadirio ya juu.

Alisema katibu mkuu aliagiza kuwe na kikao kati ya wizara na ndugu wa marehemu ili kuweka sawa changamoto hizo na kuwa na bajeti ya pamoja ambacho kilifanyika jana jioni Februari 20,2018 na kufikia muafaka.

“Wizara inapenda kuufahamisha umma kuwa taratibu nyingine za maandalizi ya mazishi zinaendelea vizuri,” amesema.

Wakati huohuo, Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dk Harrison Mwakyembe amefika nyumbani kwa dada wa marehemu Mbezi Luis kuhani msiba.

Dk Mwakyembe amesema tukio la kifo cha Akwilina ni la kusikitisha


from MPEKUZI

Comments