Mume amteka mkewe.....aamuru rafiki yake ambake kisha kammwagia tindikali

Binti wa miaka 24 mwenye mtoto mmoja ambaye ni raia wa Kenya, ameuawa kikatili baada ya kutekwa na mume wake ambaye alikuwa na rafiki yake kisha kumwambia rafiki yake huyo ambake binti huyo na baada ya mateso hayo kwa kushirikiana wakamwagia tindikali.

Lucy Ndungu aliwekewa dawa za kulevya na mumewe na ndipo alipoweza kumteka akiwa na rafiki yake, na baada ya kumbaka na kummwagia tindikali waliutupa mwili wake kando ya barabara.

Familia ya marehemu imeeleza kuwa ilimkuta Lucy anamajeraha ya kuungua kwa 75% ya mwili mzima huku hali yake ikiwa mbaya sana na hivyo akawahishwa katika Hospitali ya Taifa Kenyatta kupatiwa matibabu lakini hata hivyo akiwa kwenye matibabu hayo alifariki dunia.

Inaelezwa sababu ya mume huyo kufanya hivyo ni kwamba, walikuwa kwenye ugomvi na Lucy akaamua kuachana naye na kuondoka nyumba waliokuwa wanaishi pamoja na kukataa kurudiana na mumewe huyo jambo ambalo linadaiwa kumkasirisha mwanaume huyo.


from MPEKUZI

Comments