Rais Samia akutana na Tundu Lissu

 Rais Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu.

Taarifa iliyotolewa leo Jumatano Februari 16, 2022 na Mkurugenzi Mawasiliano ya Rais-Ikulu, Zuhura Yunus imesema kuwa mazungumzo hayo yamefanyika jijini Brussels nchini Ubelgiji baada ya Rais Samia kukubali maombi ya Lissu ya kukutana naye na kuzungumza.

“Katika mazungumzo hayo, Rais na Makamu Mwenyekiti wa Chadema Tundu Lissu walizungumza masuala mbalimbali yenye maslahi ya ustawi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania” imesema taarifa hiyo



from MPEKUZI

Comments