IGP Sirro Ataka Wazazi Waimarishe Malezi Kwa Watoto Ili Kuwa na Jamii Inayochukia Uhalifu

Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini Simon Sirro ametoa wito kwa jamii hasa wazazi nchini kuhakikisha wanaimarisha malezi ya watoto wao, jambo litalalosaidia kuwa na jamii itakayochukia uhalifu.

IGP Sirro ametoa wito huo mkoani Dodoma wakati akizungumza na baadhi ya Wakazi wa eneo la Mbande, baada ya kukagua ujenzi wa kituo cha polisi katika eneo hilo.

Amewashauri wazazi wote nchini kuendelea kuwasomesha watoto wao na kutowaacha wajiingize kwenye vitendo vya uhalifu.


from MPEKUZI

Comments