AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 69 na 70 )

MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA-
0657072588  
ILIPOISHIA

Mariam akanikumbatia kwa nguvu huku akiendelea kulia kwa uchungu. Taratibu nikaiweka bakuli la supu mezani na kuanza kunyonyana denda na Mariam, hisia za mapenzi zikaanza kupanda taratbu kati yetu, sehemu tuliyopo uzuri ni kwamba hakuna mtu yoyote. Mariam akanivua shati langu, nikamvua na yeye na tisheti
“Huu si wakati wa kufanya mapenzi, twendeni mazoezini”  
Sauti ya Livna Livba, ikatufanya tusitishe tunacho kifanya, Mariam akaniachia na kumtazama Livna kwa macho makali, akaachia msunyo mkali na kunigeukia na kuendelea kuninyonya denda jambo lillo mfanya Livna kumvuta Mariam kwa nguvu ili kuniachanisha naye.
  
ENDELEA  
Mariam hakukubali kunachia ndo kwanza akazidisha kunishika kwa mikono yake yote miwil huku  akiendelea kuninyonya denda. Livna akatutizama akatingisha kichwa kisha akatoka ndani humu na kutuacha tuendeleea na tunacho kifanya.
“Shenzi zake”
Mariam alizungumza huku akiendelea kuninyonya mate kwa kasi hatukushia hapo zaidi ya kujikuta tunaingia kwenye dibwi kubwa la mapenzi. Kila mmoja akampatia mwenzake kitu ambacho ana stahili hadi ikafikia kipindi sote tukajikuta tunafika kileleni pamoja.

“Ahahaaaa……”  
Mariam alshusha pumzi nyingi huku akinitazama usoni mwangu, taratbu akanyanyuka kwenye mapaja yangu na kila mtu akaanza kuvaa nguo zake taratbu.
“Mariam hivi tutatumia muda gani hadi kufika Korea Kaskazini?”
“Bado tuna vijiwiki kadhaa”
“Ahaa nimechoka kukaa humu ndani ya hii meli”
“Tena msimu huu tuna bahati kama ingekuwa ni msimu wa baridi kal ile ya barafu wala usinge tamani kabisa kusafiri na hizi meli”
Tukatoka katika chumba hichi huku tukiwa tumeongozana na Mariam, tukaelekea kwenye chumba cha Mariam, tukaoga kwa pamoja kisha tukabadilsha nguo.
“Hivi baba amefikira nini?”
“Kivipi?”
“Amefikira kitu gani hadi kumuweka Livna kuwa mwalimu wetu?”
“Katika hilo mimi wala bado sijalafiki, na wala hawezi kunifundisha kwa maana hapa hakuna mafunzo zaidi ya kuibiana mabwana”
Sikujibu kitu chochote zaidi ya kukaa kimya nikimtazama Mariam.

    Masaa na siku zikazidi kusonga mbele, Livna akitupa mafunzo ambayo baba ameagiza tuweze kuyafanya ili kuzidisha ujuzi katika kupambana kwetu. Kadri muda ulivyo zidi kusonga mbele ndivyo tulivyojikuta tunaimarika, japo mikasa ya hapa na pale ya Livna na Mariam kufanyiana visa vya mapenzi inatokea ila cha kumshukuru Mungu hawapigani. Baada ya wiki takribani sita tukafika nchini Korea ya Kaskazini majira ya saa mbili asubuhi. Katika maisha yangu nilisha zoea kuisikia hii ichi katika vyombo vya habari juu ya uchokozi wake katika nchi ya Korea Kusini ambapo miaka ya nyuma zilikuwa ni nchi moja kubwa zilizo kuwa zimeungana.
Bandarin tukapokwewa na sekretari wa baba aliye ongozana na walinzi wawili wa baba walio valia suti nyeusi.
“Karibuni”
Alitukaribisha wote watatu, tukaongozana nao hadi kwenye magari waliyo kuja nayo. Nikapanda gari moja na sekretari huyu huku Mariam na Livna wakipanda gari jengine la nyuma yetu na safari ikaanza kuelekea tusipo pafahamu.
“Umefanana sana na baba yako”
Sekretari alizungumza huku akiminya minya simu yake kubwa kiasi.

“Asante”
“Jina si Dany eheee?”
“Yaaa”
“Vipi Tanzania?”
“Kwema tu”
Maswali ya sekretari yakaishia hapo na ukimya ukatawala ndani ya gari. Baada ya dakika kama ishirini na tano hivi tukasimama mbele ya gorofa refu kwenda juu, ambalo kwa haraka haraka idadi ya gorofa zake zinaweza kufika mia moja na kitu hivi.
“Karibuni ndani”
Tukaongozana na sekretari. Katika sehemu ya mapokezi katika jengo hili  nikaona picha kubwa ya baba pamoja na sanamu lake lililo chongwa vizuri, huku pembeni kukiwa na herufi kubwa ya D. Katika jengo hili kuna wafanyakazi wengi wa asili  tofauti tofauti. Tukaingia kwenye lifti ambayo ina ina batani nyingi zilizo fika idadi ya batani mia moja na ishirini. Taratibu lifti ikaanza kwenda juu, huku sekretari huyu akiwa ameminya batani ya mia moja na ishirini.



from MPEKUZI

Comments