Zari atoboa siri rasmi kuachana na Diamond, amwanika vibaya “kukumbatiana na ma X kwenye public”

Kwa mara ya kwanza Zari the Bossy Lady ambaye ni mama watoto wa msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini Diamond Platinumz amefunguka kuhusu sababu za kuachana na C.E.O huyo wa kundi la Wasafi Classic Baby (WCB), amesema Diamond hakutegemea alichokipost kwani siku kabla ya kuachana walikuwa wamechuniana kwa takribani muda wa wiki tatu mfululizo, huku akiwa ameifungia simu yake, ”Block”.

Zari akiwa nchini Uingereza amepata nafasi ya kuzungumza na BBC  Swahili na kufunguka kila kitu kuhusu ishu nzima mpaka kufikia maamuzi hayo ya kutangaza kwenye akaunti yake ya instagram kuachana na Diamond katika siku ya wapendanao.

‘’Kwanza I didn’t think ali expect my post he didn’t see it coming ,nimekaa sana mda mrefu nikajifikiria vitu vingi nikasema unajua ni nini I need to post this, I  need to end this..tulikuwa tuna jaribu ku move forward kuhusu hiyo skendo eti amepata mtoto, lakini leo unasikia hivi unaona vile eti kukumbatiana na ma x kwenye public ni vitu vya kunidharirisha vitu vya kunifanya niwe very disrespected na watoto wangu’’, amesema Zari.

Zari amesema saivi hata akitembea kwa miguu kwenda kumuomba msamaha hawezi kumsamehe kwa sababu Imani juu yake imekwisha, na amesema kwa sasa hahitaji kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanaume mwingine.

Ameongezea kuwa wale wanao dhani ni kiki hawajaachana Zari amesema ni kweli wameachana na tangu kusambaa picha za Diamoni akikumbatiana na  EX wake ambaye ni Madam  Wema Sepetu, Zari amesema alimzimia simu na hawakuweza kuongea kwa wiki tatu na kisha akaamua kuchukua uamuzi wa kuachana nae.

Zari pia amezungumzia mipango yake ya hivi sasa ambapo amesema atakuwa anafanya vitu vingi ikiwemo kuendesha biashara na kazi zake ambazo amekuwa akifanya ikiwemo kusimamia shule yake iliyopo Afrika Kusini, kufanya matangazo na hivi karibuni anakuja na kipindi chake sehemu ya pili ya show yake ijulikanayo kama reality show.

Tazama Video hapa chini


from MPEKUZI

Comments