Rais Samia Kupokea Taarifa Ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ,TAKUKURU Ikulu Jijini Dodoma Kesho

Rais wa Tanzania,  Samia Suluhu Hassan kesho Jumapili Machi 28,  2021 atapokea taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) za mwaka wa fedha 2019/20.

Pia,  atapokea taarifa ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) ya mwaka 2019/20.

Taarifa iliyotolewa na mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais Ikulu,  Gerson Msigwa inaeleza kuwa tukio hilo litarushwa moja kwa moja na vyombo vya habari vya redio,  televisheni na mitandao kuanzia saa 4:00 asubuhi.

Hafla ya kupokea taarifa hiyo itafanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma.



from MPEKUZI

Comments