Wahamiaji haramu 16 kutoka Somalia Wakamatwa Njombe


Wahamiaji haramu 16 kutoka Somalia wamekamatwa kwa nyakati tofauti na vikosi vya patro vya uhamiaji vya kituo kidogo cha Makambako mkoani Njombe wakijaribu kuvuka nchini ili kufika Africa ya Kusini 


Wahamiaji 12 kati ya 16 wamekamatwa wilayani Wanging’ombe wakiwa ndani ya gari aina ya Nissan Caravan yenye nambari za usajiri T 865-DQA ambapo wameingia nchini kupitia mpaka wa Namanga wakitokea nchini Kenya huku wengine 4 wakikamatwa ndani ya Reli ya TAZARA mjini Makambako.


Akizungumzia matukio hayo mkuu wa idara ya uhamiaji mkoani humo kamishna msaidizi mwandamizi john yindi amesema jeshi limejipanga vyema kudhibiti wahamiaji haramu kwa kufanya doria masaa 24 na kwamba katika tukio la kukamatwa kwa wahamiaji 12 dereva na kondakta ambao ni watanzania walifanikiwa kutoroka na kuacha gari lao.


Kuhusu hatua zinazochukuliwa kwa wahamiaji hao Kamishna Yindi amesema tayari jitihada za kuwafikisha mahakamani zimefanyika huku pia akitoa onyo kwa mtu yeyote anayejihusisha na biashara ya kuingiza wahamiaji haramu nchini kwani atafikishwa mahakamani pia na chombo chake kutaifishwa.


Takribani Magari matatu ya watanzania wazalendo yanashikiliwa wakati kesi zikiendelea kwa kuhusika wanaotuhumiwa kuhusika na biashara hiyo chafu.



from MPEKUZI

Comments