Wenye Virusi Vya Corona Nchini Kenya Wafika 336....Ni Baada ya Wengine 16 Kuongezeka Leo

Watu 16 zaidi wameambukizwa  corona  nchini Kenya na kufanya idadi ya wagonjwa nchini Kenya kufikia 336.

Katibu wa Kudumu katika Wizara ya Afya Dkt Rashid Aman amewaambia waandishi wa habari leo Ijumaa, Aprili 24 kwamba wagonjwa hao walithibitishwa baada ya sampuli 946 kupimwa katika saa 24 zilizopita. 

Amesema Visa 11 vimetokea Nairobi huku wagonjwa wengine 5 wakiwa Mombasa.


from MPEKUZI

Comments