Maambukizi ya virusi vya Corona yapindukia 500 Jamhuri ya Demokrasia ya Congo

Visa 500 vya maambukizi vya virusi vya corona vimethibitishwa nchini Jamhuri ya Demokrasia ya Congo, watu 31 wakifariki huku watu 279 wakipona.

Kwa mijibu wa kamati iliyobuniwa kukabiliana na mlipuko huo, gereza la Ndolo limeathirika na mlipuko wa virusi hivyo, huku visa 4 vya maambukizi vikiripotiwa katika gereza hilo na wafungwa wengine 25 wakifanyiwa vipimo.

Mkoa wa Kinshasa unaongoza kwa wagonjwa wengi wa Corona, ukifuatiwa na Mkoa wa Kivu Kaskazini.

Hivi karibuni serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iliwarejesha raia wake 165 walio kuwa wanaishi ugenini na ambao walikuwa wamezuiliwa kurejea nchini humo baada ya nchi nyingi kufunga mipaka kutokana na kuibuka kwa janga la Corona.


from MPEKUZI

Comments