Msanii Bi Cheka Afariki Dunia

Msanii wa Muziki Nchini Tanzania Cheka Hija Mzee Maarufu zaidi Bi Cheka amefariki dunia mchana wa Leo Novemba 28,2019 katika Hospitali ya Mloganzila.

Kifo cha msanii huyo mkongwe kimethibitishwa na mtoto wake wa kiume, Adam Juma, ambaye amesema kuwa mama yake alikuwa akisumbuliwa na tatizo la moyo.

Familia ya marehemu inaendelea na mipango ya mazishi ambayo itaitangaza.


Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi


from MPEKUZI

Comments