Umoja wa Ulaya waurefusha tena muda wa Brexit

Umoja wa Ulaya umekubali  kuchelewesha kwa muda wa miezi mitatu Uingereza kujitoa kutoka Umoja huo hadi Januari 31.

Kiasi siku tatu kabla ya tarehe ya mwisho ya Uingereza kujitoa kutoka Umoja wa Ulaya hapo Oktoba 31, mchakato wa Brexit bado haujulikani mwelekeo wake wakati wanasiasa wa Uingereza hawako karibu ya kufikia muafaka juu ya vipi, lini na hata iwapo hatua ya kuachana na Umoja wa Ulaya itawezekana.

Mataifa 27 ya Umoja wa Ulaya yanamefikia makubaliano kuchelewesha Brexit hadi Januari 31, pamoja na uwezekano wa Uingereza kujitoa mapema iwapo bunge la Uingereza litaidhinisha makubaliano ya kujitoa.


from MPEKUZI

Comments