Twitter yapiga marufuku matangazo ya kisiasa

Jukwaa la mtandao wa kijamii Twitter limetangaza kwamba halitatangaza tena matangazo yenye muelekeo wa kisiasa.

Kiongozi mkuu ( CEO) wa Twitter, Jack Dorsey amearifu kwamba shirika hilo halitatoa tena matangazo yenye muelekeo wa kisiasa.

Dorsey amearifu kwamba uamuzi huo mpya utaanza kutumika mwishoni mwa mwezi Novemba.

Washindani wa mtandao wa kijamii wa Facebook hivi karibuni walifutilia mbali mpango wa kupiga marufuku matangazo ya siasa ya kibiashara.

Taarifa ya marufuku hiyo imeibua mgawanyiko katika kambi za kisiasa nchini Marekani zinapojiandaa katika uchaguzi wa mwaka 2020.

Brad Parscale,meneja wa kampeni ya Raisi Donald Trump, kugombea muhula wa pili, amesema marufuku hiyo ni jaribio jingine la kumnyamazisha Trump


from MPEKUZI

Comments