Rais Magufuli Na Mkewe Watoa Pole Kwa Familia Ya Mmoja Wa Waasisi Wa Vyama Vingi Nchini Marehemu Mzee James Mapalala

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa Mwanasiasa Mkongwe na mmoja wa Waasisi wa Mfumo wa Vyama vingi nchini Marehemu James Mapalala Osterbay jijini Dar es salaam aliyefariki dunia Oktoba 23,2019 katika Hospital ya Kairuki jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akimsalimia Bi. Hannah Mapalala Mke wa Marehemu James Mapalala alipokwenda na Mkewe Mama Janeth Magufuli kutoa pole nyumbani kwa Mwanasiasa Mkongwe na mmoja wa Waasisi wa Mfumo wa Vyama vingi nchini Osterbay jijini Dar es salaam aliyefariki dunia Oktoba 23,2019 katika Hospital ya Kairuki jijini Dar es salaam alipokuwa akipatiwa matibabu.


from MPEKUZI

Comments