Ndege ya pili Boeing 787-8 Dreamliner yaondoka Marekani....Kutua nchini leo mchana

Ndege mpya ya pili aina ya Boeing 787-8 Dreamliner iliyonunuliwa na Serikali kwa ajili ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) imeondoka nchini Marekani jana Ijumaa, Oktoba 25, 2919 kuja Dar es Salaam Tanzania.

Ndege hiyo kubwa yenye uwezo wa kuchukua abiria 262 inatarajiwa kutua katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam leo mchana Oktoba 26, 2019.

Ndege hiyo itapokelewa na wananchi wakiongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Hii inakuwa ndege ya 8 kati ya ndege 11 zilizonunuliwa na Serikali kwa lengo la kuimarisha Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kukuza utalii na uchumi.


from MPEKUZI

Comments