Kampuni Ya China Yawekeza $1 Bilioni Sekta Ya Kilimo Tanzania

Kampuni ya Super Agri Technology ya China imesaini makubaliano na kampuni ya Tanzania Agriculture Export Process Zone kuwekeza $1 bilioni katika sekta ya kilimo na usindikaji kwa kipindi cha miaka mitano.

Makubaliano hayo yamesainiwa katika mkutano wa China-Africa Economic& Trade Expo yanayofanyika mji wa Changsha.

Katika hafla hiyo kampuni ya Tanzania Agriculture Export Process Zone iliwakilishwa na Afisa wa Taasisi ya Sekta Binafsi TPSF, Lilian Ndosi.


from MPEKUZI

Comments