Jaguar Anyimwa Tena Dhamama

Mbunge wa Jimbo la Starehe Kenya Jaguar ataendelea kusalia rumande kwa siku 5 zaidi baada ya Mahakama kuagiza Mbunge huyo aendelee kushikiliwa katika kituo cha Polisi mpaka Jumatano ya wiki ijayo kuruhusu uchunguzi zaidi juu ya kesi yake.

Jaguar aliyekuwa mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi,  Sinkyani Tobiko, anakabiliwa na  mashtaka ya kutoa kauli ya uchochezi dhidi ya wafanyabiashara wa kigeni nchini humo jijini Nairobi katika Barabara ya Kirinyaga alipowataka wafanyabiashara hao kuondoka nchini humo la sivyo watashambuliwa.


from MPEKUZI

Comments