Rais Magufuli na Amiri Jeshi Mkuu atunuku Kamisheni kwa Maafisa wapya 146 wa JWTZ Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini, Dkt John Magufuli, leo Machi 30, 2019, amewatunuku Kamisheni Maofisa Wanafunzi wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Rais Magufuli amewatunuku Kamisheni katika cheo cha Luteni USU maafisa hao wanafunzi ambao idadi yao ilikua 146.

Hafla ya utunukiwaji kamisheni kwa Maafisa hao imefanyika katika viwanja wa Ikulu jijini Dar es Salaam.



from MPEKUZI

Comments