DC Jokate Mwegelo Amuomba Radhi Pierre Liquid

Baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda kumkosoa Mchekeshaji aliyejizolea umaarufu kwenye vyombo vya habari pamoja na mitandao, Pierre Maarufu kama Mzee wa Liquid ,Mkuu wa wilaya ya Kisarawe Jokate Mwegelo amemuomba Radhi kwa tukio hilo.

 
Katika hafla iliyoandaliwa na Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe, Jokate Mwegelo yenye malengo ya kutokomeza Zero katika wilayani humo, Makonda alisema kwamba watu wa 'hovyo' kama Pierre hawapaswi kupewa nafasi kwenye vyombo vya habari.

"Wakina mama kama hawa wanaojituma na kuhangaika kwa ajili ya watoto, wao ndio tuwape kipaumbele, sio hawa walevi walevi kama akina Pierre. Yaani unakuwa na taifa ambalo watu wa hovyo ndio wanakuwa maarufu”, Alisema Paul Makonda.


Hata hivyo, Mkuu wa Wilaya Jokate kupitia ukurasa wake Instagram amemuomba Radhi Pierre na kumkaribisha Kisarawe ikiwa ni pamoja na kumpatia fursa ya kutengeneza samani za shule mpya inayotegemewa kujengwa katika Wilaya hiyo. 

==Haya ni Maneno ya Jokate

"Hakuna maneno Muhimu na Machache katika ustawi wa maisha ya Binadamu kama Tafadhali, Asante na Samahani.

Katika Dhifa niliyoiandaa jana, nilialika watu wengi, Wanasiasa, Taasisi za Kiserikali, Mabalozi, Wafanyabiashara, Wajasiriamali, Wasanii, Wadau wa Burudani N.k.

Na Makusudio ya yote hayo wote tunayajua, ni kutafuta MOTISHA juu ya ELIMU ya Mtoto wa kike, Kisarawe na kote nchini.
Na kwangu mimi na Wilaya nzima ya Kisarawe wote waliofika jana ni muhimu sana sana kwangu na kwetu.

Kipekee kabisa nimshukuru @officialpiere_liquid wako watu maarufu wengi mno tuliowaalika lakini hawakufika. Ila wewe ulichukua muda wako kuhamamisha na kufika na zaidi ya hapo ukatoa mchango wa TSH LAKI MOJA!!! Hukuja kuuza sura tu!! Nasema ASANTE SANA.

Wana Kisarawe tunakupenda na tunakukaribisha kuwekeza Kisarawe uanzishe hata mgahawa tutakusaidia kupata eneo. Lakini pia nimesikia ni mtengeneza mzuri sana wa furniture. Hii Shule tunayoenda kujenga inahitaji madawati Naomba tufanye kazi nawewe katika hii fursa. Tuangalie namna japo kidogo tukuwezeshe.

Tunasema Karibu Kisarawe Ukae. Kisarawe Kunogile. Tunasema Samahani kwa kukwazika lakini zaidi Asante Sana kwa kushiriki kwenye #TokomezaZeroKisarawe
#ElimuItabakiKuwaJuuKileleni
 #KisaraweMpya

Ubarikiwe!!!" - DC Jokate Mwegelo


from MPEKUZI

Comments