Breaking News: Mahakama Kuu Yatupilia Mbali Maombi ya Joshua Nassari Kupinga Kuvuliwa Ubunge

Mahakama Kuu kanda ya Dodoma imetupilia mbali maombi ya Joshua Nassari ya kupinga kitendo cha Spika wa Bunge kumvua ubunge wa Arumeru Mashariki kutokana na utoro bungeni

Akisoma maamuzi hayo leo Ijumaa Machi 29, 2019 Jaji wa Mahakama Kuu Dodoma, Latifa Mansour   ametumia kifungu cha 5 (4) kuwa Nassari alipaswa kupeleka malalamiko yake kwa Katibu wa bunge wala si kama alivyofanya.

Kifungu kingine kilichombana Nassari  ni cha kanuni ya 146 (2) kwamba alijifukuzisha mwenyewe kwa kutohudhuria vikao vitatu mfululizo vya Bunge bila taarifa.


from MPEKUZI

Comments