Mwili wa Ruge Kuwasili Nchini Ijumaa ya March 1, 2019

Mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba unatarajiwa kuwasili nchini  Ijumaa ya  Machi 1,2019 na utazikwa Bukoba, mkoani Kagera wiki ijayo.

Annik Kashasha ambaye ni msemaji wa Familia ya Mutahaba amesema Leo Jumatano February 27 kuwa  kama mambo yakienda kama yalivyopangwa,  wakazi wa Dar es Salaam watatoa heshima za mwisho na kumuaga Ruge siku ya Jumamosi,March 2.

Baada ya hapo Familia imeamua kwamba Ruge atakwenda kuzikwa nyumbani kwao huko Bukoba siku ya Jumatatu ya March 4, 2019.


from MPEKUZI

Comments