Spika Ndugai : Bila Viboko Shuleni Mambo Hayaendi

Spika wa Bunge, Job Ndugai, amesema bila viboko shuleni mambo hayaendi vizuri.

Spika amesema hayo leo Alhamisi Januari 31, bungeni jijini Dodoma baada ya Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, William Ole Nasha, kusema viboko vitaendelea kutumia shuleni.

Ole Nasha alikuwa akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Zainab Katimba.

Katika swali lake Katimba alitaka kujua kama adhabu ya viboko inaongeza kiwango cha ufaulu.

Akijibu swali hilo, Ole Nasha amesema Serikali itaendelea kusisitiza matumizi sahihi ya adhabu kwa wanafunzi ili kuleta tija katika ufundishaji na ujifunzaji.


from MPEKUZI

Comments